Header

MIFUGO NA UVUVI JOBS JULY 2013

TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI

Serikali kupitia Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi imepanga kuajiri Wataalam wa Kada za Mifugo na Uvuvi katika mwaka 2012/2013. Hivyo, tunapenda kuwatangazia Watanzania wote wenye sifa watume barua za maombi ya kazi zifuatazo:


1.  Daktari Mifugo Mkufunzi Daraja la II (Veterinary Tutor II)  Nafasi 1

(a)      Sifa za waombaji
Waombaji wawe wamehitimu Shahada ya Sayansi ya Tiba ya Mifugo kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine au Chuo kingine kinachotambuliwa na Serikali na wawe wamesajiliwa na Bodi ya Madaktari wa Mifugo Tanzania.

(b)      Majukumu
  • Kutafsiri mihutasari ya mafunzo kwenye masomo;
  • Kuandaa mtiririko wa kila somo (lesson plan) kwa upande wa nadharia na vitendo;
  • Kufundisha kozi za stashahada na astashahada kwa upande wa nadharia na vitendo;
  • Kuandaa na kupanga somo la vitendo na kusimamia wanachuo wakati wa kujifunza;
  • Kupima maendeleo ya wanachuo kwenye mitihani kwa kipindi chote kinaehohusika na kutunza alama zao;
  • Kupima maendeleo ya wanachuo kwa kushirikiana na madaktari/maofisa mifugo wa wilaya, viwandani wakati wa mafunzo kwa vitendo (Field Practicals).

(c)       Mshahara wa watumishi wa Serikali ngazi ya TGS F

2.   Daktari Utafiti Mifugo Daraja la II (Veterinary Research                         Officer II)  Nafasi 2

(a)      Sifa za waombaji
Waombaji wawe wamehitimu Shahada ya Sayansi ya Tiba ya Mifugo kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine au Chuo kingine kinachotambuliwa na Serikali na wawe wamesajiliwa na Bodi ya Madaktari wa Mifugo Tanzania.


(b)      Majukumu
  • Kujifunza na kumudu mbinu na taratibu za utafiti wa afya na maradhi ya mifugo;
  • Kuweka kumbukumbu za utafiti;
  • Kusaidia kuendesha semina za maonyesho ya ufugaji bora;
  • Kuandaa mapendekezo  ya Utafiti (Reserach Proposal) kwa kushirikiana na Daktari Utafiti Mifugo anayemsimamia;
  • Kufanya utafiti chini ya usimamizi wa Daktari Utafiti Mwandamizi;
  • Kukusanya na kuchambua takwimu za utafiti unaoendelea na;
  • Kuchapisha taarifa na makala za Utafiti.

 (c)      Mshahara wa watumishi wa Serikali ngazi ya TGRS C       

3.   Afisa Utafiti Mifugo Daraja la II (Livestock Research  Officer II)      Nafasi 5

(a)      Sifa za waombaji
Waombaji wawe wamehitimu Shahada ya Sayansi ya Wanyama kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine au Chuo kingine kinachotambuliwa na Serikali.

(b)      Majukumu
  • Kujifunza na kumudu mbinu na taratibu za utafiti wa mifugo/ndorobo.
  • Kufanya utafiti chini ya usimamizi wa Afisa Utafiti Mwandamizi.
  • Kuandika na Kuweka kumbukumbu za utafiti.
  • Kusaidia kuendesha semina na maonyesho ya ufugaji bora.
  • Kuandaa mapendekezo ya utafiti (Research Proposals) kwa kushirikiana na Afisa Utafiti Mifugo anayemsimamia.
  • Kufanya kazi zo zote kama atakavyoelekezwa na mkuu wake wa kazi

Mshahara wa watumishi wa Serikali ngazi ya TGRS A


4.   Mkufunzi Mifugo Daraja la II (Livestock Tutor II)          Nafasi 1
(a)      Sifa za waombaji
Waombaji wawe wamehitimu Shahada ya Sayansi ya Mifugo au Elimu, Mafunzo na Ugani kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine au Chuo kingine kinachotambuliwa na Serikali.

(b)      Majukumu
  • Kutafsiri mihutasari ya mafunzo kwenye masomo.
  • Kuandaa mtiririko wa kila somo (lesson plan) kwa upande wa nadharia na vitendo.
  • Kufundisha kozi za stashahada na astashahada kwa upande wa nadharia na vitendo.
  • Kuandaa na kupanga somo la vitendo na kusimamia wanachuo wakati wa kujifunza.
  • Kupima maendeleo ya wanachuo kwenye mitihani kwa kipindi chote kinachohusika na kutunza alama zao.
  • Kupima maendeleo ya wanachuo kwa kushirikiana na maofisa mifugo wa wilaya, viwandani wakati wa mafunzo kwa vitendo (Field Practicals).

Mshahara wa watumishi wa Serikali ngazi  ya TGS D


5.   Afisa Mifugo Msaidizi Daraja la II (Livestock Field Officer II) Nafasi 16

 (a)     Sifa za waombaji `
Waombaji wawe wamehitimu Elimu ya kidato cha IV au cha VI wenye Stashahada (Diploma) ya Mifugo kutoka vyuo vya Mifugo (Livestock Training Institute – LITI) au Vyuo vingine vinavyotambuliwa na Serikali.


(b)      Majukumu
  • Kufanya uchunguzi wa magonjwa ya mifugo kwa wafugaji wa eneo lake;
  • Kukusanya takwimu za nyama na mazao yatokanayo na mifugo kama ngozi na kuandika ripoti;
  • Kushirikiana na Wakaguzi wa Afya, kukagua nyama na usafi wa machinjio mara kwa mara;
  • Kutibu na kutoa chanjo za magonjwa ya mifugo chini ya usimamizi wa Daktari wa Mifugo na kushauri wafugaji jinsi ya kukinga mifugo dhidi ya magonjwa;
  • Kusimamia uchanganyaji wa dawa ya josho;
  • Kushauri wafugaji juu ya mbinu bora za kuzalisha maziwa na utunzaji wa ndama;
  • Kusaidia katika uhamilishaji (Artificial Insermination) na Uzalishaji (Breeding) wa mifugo kwa ujumla;
  • Kukusanya takwimu za maendeleo ya mifugo katika eneo lake na;
  • Kushauri na kusimamia ujenzi wa majosho, machinjio, vibanio na miundombinu inayohusiana na ufugaji bora.

( c )     Mshahara wa watumishi wa Serikali ngazi  ya TGS C


6.   Mhandisi Baharini  II (Marine Engineer II) Nafasi 1

(a)      Sifa za waombaji
Waombaji wawe wamehitimu Shahada/Stashahada ya Juu ya Uhandisi kutoka Vyuo Vikuu vinavyotambuliwa na Serikali.

(b)      Majukumu
  • Kusimamia ufungaji wa mitambo katika vyombo vya uvuvi;
  • Kushauri juu ya aina za vyombo/mitambo inayostahili kuendeleza uvuvi;
  • Kusimamia matengenezo ya vyombo vya uvuvi na;
  • Kusimamia uendeshaji wa mitambo ya vyombo vya baharini.

(c )      Mshahara wa watumishi wa Serikali ngazi  ya TGS E

7.   Mkunfuzi wa Mifugo Msaidizi Daraja la II (Assistant Livestock Tutor  II) Nafasi 1

 (a)     Sifa za waombaji `
Waombaji wawe wamehitimu Elimu ya kidato cha IV au cha VI wenye Stashahada (Diploma) ya Mifugo kutoka vyuo vya Mifugo (Livestock Training Institute – LITI) au Vyuo vingine vinavyotambuliwa na Serikali.

(b)      Majukumu
  • Kuandaa mtiririko (Lesson Plan) wa somo;
  • Kufundisha Kozi ya Astashahada ya Mifugo kwa Wanafunzi na wafugaji;
  • Kusimamia  masomo ya vitendo chini ya usimamizi wa Mkufunzi Mkuu wa somo;
  • Kuandaa na kupanaga vifaa kwa ajili ya somo la vitendo;
  • Kuwapima wanachuo wakati wa mazoezi ya somo la vitendo na
  • Anaweza kuteuliwa kuwa Mkuu wa Kitengo (Dairy,Poultly,maabara, museum)

( c ) Mshahara wa watumishi wa Serikali ngazi  ya TGS C


8.   Fundi Sanifu Maabara  za Mifugo Daraja la II (Veterinary Laboratory Technician  II) Nafasi 2

 (a)     Sifa za waombaji
Waombaji wawe wamehitimu Elimu ya kidato cha VI wenye Stashahada (Diploma) katika fani ya Fundi Sanifu Maabara (Mifugo) kutoka Chuo cha Mifugo (LITI) au vyuo vingine vinavyotambuliwa na Serikali.

(b)      Majukumu
  • Kukusanya sampuli kwa ajili ya uchunguzi wa maabara;
  • Kuwasaidia wataalam kuandaa vifaa vya uchunguzi;
  • Kutunza takwimu za uchunguzi;
  • Kutunza usafi wa maabara na vyombo vilivyomo;

( c )     Mshahara wa watumishi wa Serikali ngazi  ya TGS C


9.   Afisa Uvuvi Msaidizi II (Asistant Fisheries Officer II) Nafasi 2


(a) Sifa za waombaji
Waombaji wawe wamehitimu Elimu ya kidato cha VI wenye Stashahada (Diploma) Uvuvi au Uhifadhi wa Samaki na Masoko (Fish Processing & Marketing) kutoka vyuo vya uvuvi vya Mbegani, Kunduchi, Nyegezi au vyuo vingine vinavyotambuliwa na Serikali.


(b) Majukumu
  • Kutengeneza, Kushona, Kutunza na Kukarabati zana za uvuvL
  • Kutunza na kuangalia mabwawa ya samaki
  • Kutega mitego Ziwani au Baharini.
  • Kutengeneza nyavu ndogo ndogo.
  • Kuwapa chakula samaki katika mabwawa.
  • Kuvua samaki katika mabwawa.
  • Kutoa ushauri kwa wavuvi kuhusu mbinu mbalimbali za uvuvi.
  • Kukusanya takwimu za uvuvi kutoka kwenye vituo vya kupokelea samaki.
  • Kutoa ushauri juu ya uhifadhi wa samaki na mbinu za usambazaji na uuzaji wa mazao yatokanayo na samaki.
  • Kuwaelimisha wananchi juu ya ufugaji wa samaki na mambo muhimu I

( c )     Mshahara wa watumishi wa Serikali ngazi  ya TGS C

10.        Mteknolojia wa Samaki  II (Fish Technologist II) Nafasi 1

(a)      Sifa za waombaji

Waombaji wawe wamehitimu Shahada ya Sayansi ya Chakula (Food Science and Food Nutrition, Food Technology, Microbiology) kutoka Vyuo Vikuu vinavyotambuliwa na Serikali.


(b)      Majukumu

  • Kutoa ushauri juu ya utayarishaji, utengenezaji, ukaushaji na uhifadhi wa samaki na mazao yatokanayo na uvuvi;
  • Kusimamia na kushauri juu ya Kanuni za uthibiti ubora wa Samaki na mazao yake;
  • Kutoa ushauri juu ya matumizi mbalimbali ya samaki kama chakula bora katika viwanda na maeneo mengine;
  • Kudhibiti ubora wa samaki katika mialo;
  • Kuthibiti usafi katika maeneo ya kupokelea samaki na;
  • Kukagua nyaraka mbalimbali zinazotakiwa kutunzwa melini na viwandani.

(c )      Mshahara wa watumishi wa Serikali ngazi  ya TGS D



MAMBO YA KUZINGATIA

(i)              Barua za maombi zimbatane na Maelezo Binafsi  (CV), picha ndogo za 2 ukubwa wa pasipoti, cheti cha kuzaliwa, vyeti vya kuhitimu elimu ya Sekondari na Shahada;
(ii)             Waombaji wawe na umri usiozidi miaka 45;
(iii)            Wahitimu walioajiriwa Serikalini hawaruhusiwi kuomba nafasi hizi kwa sababu tayari wana ajira;
(iv)           Wahitimu waliotuma maombi yao kabla ya tangazo hili wanashauriwa kutuma maombi upya;
(v)            Barua zote za maombi ziwasilishwe katika muda wa siku saba kuanzia tarehe ya kwanza ya kutolewa tangazo hili;
(vi)           Tangazo hili linapatikana kwenye Tovuti ya Wizara www.mifugouvuvi.go.tz na;
(vii)          Barua zote zitumwe kwa:


Katibu Mkuu,
Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi,
S.L.P 9152,

DAR ES SALAAM.